Vigezo ya Kujiunga

Stashahada ya hali ya hewa(NTA Level 6)

Dirisha la Udahili ngazi ya stashahadi(Diploma) limefunguliwa kwa wahitimu wenye cheti ngazi ya Astashahada ya hali ya hewa (NTA Level 5)

Astashahada ya hali ya hewa (NTA Level 5)

Dirisha la Udahili ngazi ya astashahada (Cheti) limefunguliwa kwa wahitimu wenye cheti cha elimu ya sekondari(A’ Level) katika kada ya PCM na PGM wenye ufaulu katika masomo ya Fizikia na Hisabati. Au wahitimu wawe na astashahada ya Awali ya hali ya hewa (NTA Level 4)

Astashahada ya Awali ya hali ya Hewa(NTA level 4)

Dirisha la Udahili ngazi ya astashahada (Cheti cha Awali) limefunguliwa kwa wahitimu wenye cheti cha elimu ya sekondari(O’Level) wenye ufaulu wa alama ’D’ katika masomo manne ikiwemo Hesabu na Fizikia


Jinsi ya kujiunga :


Mwombaji anatakiwa kupakua fomu ya maombia kupitia https://www.nmtc.ac.tz/uploads/publications/en1684934409-APPLICATION%20FORM%202023-2024%20UPLOAD.pdf na kutuma fomu pamoja na viambatanisho kupitia barua pepe ya Chuo iliopo kwenye fomu ya maombi.